Taasisi zilizo chini ya wizara ya fedha zatakiwa kujitangaza

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, anayeshughulikia Huduma za Hazina, Bi. Jenifa Christian Omolo, ameziagiza taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kutangaza utekelezaji wa majukumu yao ili umma wa watanzania ujue.

Bi. Omolo ameyasema hayo Oktoba 25, 2023, wakati akifungua Kongamano la Wakuu wa Vitengo vya Mawasiliano wa Taasisi za Wizara ya Fedha na Wahariri wa Vyombo vya Habari, mjini Morogoro.

“Taasisi zetu tumeziunganisha na masuala ya kiuchumi yanayohusu watu, nendeni mkajitangaze, mkijitangaza watu watajenga imani kwenu.” Amesema na kuongeza..Tumieni teknolojia katika kuwasiliana kwa sababu habari ni biashara na biashara ni fedha na fedha ni uchumi.” Amesisitiza Bi. Omolo.

Share: