Dkt. biteko afungua jengo la ofisi mamlaka ya maji zanzibar

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amefungua Jengo la Afisi ya Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) lililoko eneo la Madema, Zanzibar na kupongeza mafanikio na ushindi wa kufanikisha miradi hiyo muhimu kwa maendeleo ya Zanzibar.

Dkt Biteko amesema, kuelekea Kilele cha Mapinduzi ya Zanzibar, watu waliopewa dhamana ya kusimamia miradi hiyo ambayo Serikali imepeleka fedha nyingi, wafanye kazi kwa uaminifu kwani watatatoa hesabu si tu kwa waliowaweka madarakani, au Wananchi bali kwa Mwenyezi Mungu, hivyo wafanye kazi kwa uaminifu mkubwa.

Aidha, alipongeza pia Wizara ya Maji kwa kuwajali wafanyakazi wake kwa kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa wafanyakazi wake ikiwa ni kuwajengea jengo lililoondoa changamoto ya nafasi kwa wafanyakazi hususani kwenye jengo la awali.

Dkt Biteko amesema, ujenzi wa Jengo Hilo la ghorofa 4 lililogharimu kiasi cha Dola za kimarekani Milioni 92.18 kama mkopo toka Benki ya Exim Kutoka India kwa ushirikiano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, unahusisha Ofisi za wafanyakazi, Maabara, Ukumbi wa Mikutano, Maegesho na Ukumbi wa Mazoezi na kuipongeza Wizara ya Maji, Nishati na Madini kwa kujenga jengo lenye hadhi na ubora wa hali ya juu.

“Zanzibar ndio nchi pekee Afrika Mashariki, na pengine Duniani kwa kuwajali wananchi wake kwa kuwapatia Maji ambayo wanayachagia na sio kulipia Maji” Alisisitiza Mhe. Kaduara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Mhandisi. Dkt. Salha Mohamed, amesema ujenzi wa jengo hilo ulianza mwezi Machi, 2021 ikiwa ni sehemu ya uhuishaji na ustawishaji Maji Zanzibar chini ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maji chini ya miradi mitatu ambapo wa kwanza ni wa Mfenesini na Dole unaogharimu Dola za Kimarekani Milioni 26,167, 200, Awamu ya pili unaogharimu kiasi cha Dola za kimarekani Milioni 27,740,731, ambao umejenga matanki makubwa sita, matatu chini, na matatu juu, na ya tatu ni ile inayohusiaha Masongini, Kwarara na ZAWA kwa ujenzi wa matanki matano, na unagharimu kiasi cha zaidi ya milioni 35.

Share: