West midlands uingereza: police wakumbana na adhabu kwa kumvua nguo za ndani msichana mafunzoni

Mahakama nchini Uingereza imemuamuru afisa wa polisi kulipwa fidia ya pauni 30,000 kwa kumvua nguo za ndani wakati wa mazoezi baada ya muathiriwa kusema kuwa 'aliokolewa'.

Rebecca Kalam alikuwa ameishutumu idara ya polisi kwa kutumia lugha ya ngono na matusi . Kesi hiyo iliendeleana akashinda.

Katika mahojiano ya kipekee na Chanzo cha Habari BBC, Rebecca Kalam alisema 'amehuzunishwa' kwamba unyanyasaji na ubaguzi aliokumbana nao haukukomea kwake tu.

"Polisi wa West Midlands wamekubali kuwajibika kikamilifu kwa makosa yake mengi, lakini hakuna ulinzi wa wazi au mabadiliko ya miendendo kwa maafisa wake wa kike," alisema.

Rebecca Kalam ni mkaguzi wa zamani wa uchunguzi na alijiunga na jeshi la polisi mnamo Septemba 2008.

Alijiunga na Kitengo cha udhibiti wa Silaha mnamo 2012 na kustaafu kwa sababu za kimatibabu mnamo Julai 2023.

Share: