
Daraja la J.P. Magufuli (pia likijulikana kama Kigongo–Busisi Bridge) lilizinduliwa rasmi tarehe 19 Juni 2025 huko Mwanza na Rais Samia Suluhu Hassan, tukio lililotangazwa na Waziri Ujenzi Abdallah Ulega na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,huku shamra shamra za wananchi na wadau mbali mbali zikisheheni .
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Daraja la JP Magufuli (Kigongo-Busisi) lenye urefu wa km 3.0 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 1.66 katika eneo la Kigongo, Misungwi mkoani Mwanza tarehe 19 Juni, 2025. Daraja hilo ambalo ni sehemu ya barabara ya Usagara-Sengerema-Geita ni sehemu ya barabara kuu inayoanzia Sirari hadi Mtukula na ujenzi wake ulianza rasmi mwezi Februari, 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisogeza kitambaa kuashiria ufunguzi wa Daraja la J.P Magufuli (Kigongo-Busisi) lenye urefu wa km 3.0 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 1.66 katika eneo la Kigongo, Misungwi mkoani Mwanza tarehe 19 Juni, 2025. Daraja hilo ambalo ni sehemu ya barabara ya Usagara-Sengerema-Geita ni sehemu ya barabara kuu inayoanzia Sirari hadi Mtukula na ujenzi wake ulianza rasmi mwezi Februari, 2020.
Shamrashamra za ufunguzi wa Daraja la JP Magufuli (Kigongo-Busisi) lenye urefu wa km 3.0 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 1.66 katika eneo la Chuo cha ufundi Kalwande, Kigongo wilayani Misungwi mkoani Mwanza tarehe 19 Juni, 2025.
Fahamu ya kuwa Jumla ya gharama: Zaidi ya Sh. 700 bilioni (~USD 300 milioni), zote zikitokana na hazina ya serikali .Serikali ililipia awali karibu Sh. 150 bilioni, ikifuatiwa na malipo ya jumla ya takriban Sh. 611–700 bilioni, Daraja hili lina manufaa ya fwatayo,Manufaa ya Daraja mengi yakiwemo , Kupunguza muda wa safari: Kutoka saa 2 kwa vivuko hadi dakika 3–5 kwa magari .
Kuongeza shughuli za kiuchumi: Kukuza biashara, usafirishaji, na maendeleo katika Mkoa wa Kanda ya Ziwa, hasa Mwanza, Geita, Sengerema na maeneo jirani,Kujumuisha Mkoa wa Geita: Kuondoa utegemezi wa vivuko, na kuwaunganisha wengine kupitia barabara kuu ya T4 (Usagara‑Sengerema‑Geita) .