Rais samia suluhu afupisha safari ya dubai

Rais Samia Suluhu ambaye yupo Dubai kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP28) ameamua kufupisha safari hiyo ili kurejea nchini kushughulikia janga la mafuriko wilayani Hanang, Manyara.

Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali itagharamia mazishi ya wote waliofariki kutokana na mvua kubwa iliyotokea na kusababisha mafuriko katika Wilaya ya Hanang mkoani Manyara.

Aidha, ameelekeza majeruhi wote wanaohudumiwa katika hospitali mbalimbali kupata matibabu yanayostahili kwa gharama za Serikali.


Share: