Mwanamke wa australia ashtakiwa kwa kuiba gari lililokuwa limebeba donati 10,000

Mwanamke mmoja nchini Australia ameshtakiwa kwa kuiba gari la kubebea mizigo lililokuwa na donati 10,000 za Krispy Kreme.

Gari hilo lilitoweka kwenye kituo cha petroli katika kitongoji cha Sydney saa za mapema tarehe 29 Novemba.

Polisi walipata gari hilo likiwa limetelekezwa wiki moja baadaye - pamoja na maelfu ya donati zilizoharibika - kwenye maegesho ya magari.

Walimkamata mwanamke huyo, 28, siku ya Alhamisi. Alinyimwa dhamana na anakabiliwa na mashtaka ikiwa ni pamoja na wizi wa gari na kuendesha gari licha ya kukosa leseni.

Picha za CCTV za tukio hilo zinadaiwa kumuonyesha mwanamke huyo akiwa kwenye kituo cha huduma mwendo wa saa 04:00 kwa saa za eneo (17:00 GMT mnamo 28 Novemba) kabla ya kuingia ndani ya gari hilo la kusafirisha bidhaa ambalo halikuwa na mtuna kuanza kuliendesha.

Haijulikani ikiwa alijua gari hilo lilikuwa na donati 10,000 ikiwa ni pamoja na zenye mapambo ya Krismasi.

Share: