Maduka yaanza kufunguliwa katika mji wa katesh - hanang

Zoezi la kurejesha mji wa Katesh katika hali yake ya awali ili kuwezesha shughuli za uzalishaji kuendelea, imefikia katika hatua nzuri ambapo asubuhi ya leo tarehe 07 Disemba 2023 Maduka na huduma nyingine zimeanza kurejea katika hali ya kawaida.

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa akishirikiana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Jenista J. Mhagama pamoja na viongozi wengine wameendelea kupiga kambi ya kusimamia uzoaji wa tope usiku na mchana ikiwa ni pamoja na kusafisha mji wa Katesh wilayani Hanang.

Share: