Kenya: paul mackenzie ashtakiwa kwa kuua bila kukusudia

Kiongozi wa kanisa la ekufunga hadi kufa nchini Kenya Paul Mackenzie ameshtakiwa kwa makosa 238 ya kuua bila kukusudia, pamoja na mkewe na watu wengine 93 wanaodaiwa kuwa washirika wake.

Mashtaka hayo ya ziada yanakuja baada ya Bw Mackenzie na watu wanaoshukiwa kuwa washirika wake kushtakiwa kwa ugaidi wiki jana.

Anadaiwa kuwahimiza waumini wa Kanisa lake la Good News International kuhamia Shakahola, msitu wa mbali katika pwani ya Kenya, na kufunga hadi kufa ili "kukutana na Yesu".

Miili ya watu 429 wakiwemo watoto imefukuliwa kutoka maeneo ya makaburi katika msitu huo.

Wengi wao walionyesha dalili za njaa, lakini wengine - watoto kati yao - wanaweza kuwa walivamiwa.

Waathiriwa 238 waliuawa arehe zisizojulikana kati ya Januari 2021 na Septemba 2023 huko Shakahola, ripoti ya vyombo vya habari vya ndani, ikitoa hati za korti.

Bw Mackenzie na washukiwa wengine walikana mashtaka walipofikishwa katika mahakama moja katika mji wa pwani wa Mombasa siku ya Jumanne.

Bw Mackenzie amekuwa kizuizini tangu kukamatwa kwake Aprili mwaka jana.

Share: