Kamati za maafa zitoe elimu kwa wananchi

Kamati za maafa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi zimekumbushwa kutoa elimu kwa jamii katika maeneo yao kuhusu namna ya kujiandaa na kukabiliana na maafa pamoja na kurejesha hali pindi majanga yanapotokea.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mhe. Shaibu Ndemanga wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kuzijengea uwezo kamati za maafa katika Manispaa hiyo kuhusu Upunguzaji wa madhara ya maafa katika jamii yaliyofanyika Ukumbi wa mikutano wa DDC mkoani Lindi .

Mkuu wa Wilaya hiyo amesema mafunzo hayo yanafanyika wakati muafaka ikiwa ni mwendelezo wa mikakati ambayo imekuwa ikifanywa na Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu katika kupunguza madhara ya maafa kwa kuhakikisha huduma za dharura zinatolewa kwa wakati ikiwa ni pamoja na kuokoa watu na mali na kuwahimiza wadau wa kamati hizo kufahamiana ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Share: