Hali inaelezwa sio shwari katika mpaka wa lebanon na israel

Israel na kundi la Hezbollah linaloungwa mkono na Iran wamekuwa wakirushiana risasi tangu vita vya Gaza vilipozuka miezi miwili iliyopita katika uhasama wao mbaya zaidi tangu kuzuka kwa mzozo wa mwaka 2006. Vurugu hizo kwa kiasi kikubwa zimeshuhudiwa katika eneo la mpakani.

Vurugu ziliongezeka katika mpaka wa Lebanon na Israel siku ya Jumapili wakati Hezbollah iliporusha vilipuzi kutumia ndege zisizokuwa na rubani na makombora yenye nguvu katika maeneo ya Israel, na mashambulizi ya anga ya Israel yalitikisa miji kadhaa na vijiji kusini mwa Lebanon.

Israel na kundi la Hezbollah linaloungwa mkono na Iran wamekuwa wakirushiana risasi tangu vita vya Gaza vilipozuka miezi miwili iliyopita katika uhasama wao mbaya zaidi tangu kuzuka kwa mzozo wa mwaka 2006. Vurugu hizo kwa kiasi kikubwa zimeshuhudiwa katika eneo la mpakani.

Shambulio la anga la Israel katika mji wa Aitaroun liliharibu nyumba tano na nyingine nyingi, alisema Ali Hijazi, afisa wa eneo hilo. Uingiliaji wa Imani ya kidini ulizuia mtu yeyote kuuawa. Wanawake watatu na wanaume wawili walijeruhiwa, aliliambia shirika la habari la Reuters. Jeshi la Israel halikujibu mara moja kufuatia ombi la kutoa maoni juu ya tukio hilo.

Mwanasiasa mwandamizi wa Hezbollah Hassan Fadlallah, katika taarifa yake kwa shirika la habari la Reuters, amesema mashambulizi ya anga ya Israel, yaliongezeka upya ambapo kundi hilo lilikuwa likijibu aina mpya ya mashambulizi, iwe ni kwa mazingira ya silaha zilizotumika au maeneo yaliyolengwa.

Share: