Ghana: mtu mmoja amethibitishwa kufariki huku wengine wakipata majeraha kufuatia ajali iliyohusisha magari ya msafara wa rais nana akufo addo

Mtu mmoja amethibitishwa kufariki huku wengine wakipata majeraha tofauti tofauti kufuatia ajali iliyohusisha magari kadhaa ya msafara wa Rais Nana Akufo Addo siku ya Jumapili.

Chanzo kamili cha ajali hiyo hakijajulikana, Msafara huo ulikuwa ukirejea kutoka Kumasi kuelekea mji mkuu, Accra.

Dereva wa mojawapo ya magari hayo alipoteza maisha, huku wengine katika usalama wa rais wakipata majeraha mbalimbali na wamepata matibabu ya awali katika hospitali iliyo karibu.

Wamesafirishwa hadi Accra kwa matibabu zaidi.

Baadhi ya magari pia yameharibika kiasi cha kutoweza kurekebishwa. Taarifa iliyotolewa na ofisi ya rais ilionyesha kuwa Rais Akufo Addo yuko salama na alisafiri kurejea Accra kwa helikopta ya kijeshi.

Barabara kuu ya Accra Kumasi ni ya njia moja, na ajali hutokea mara kwa mara, mara nyingi husababisha vifo.

Share: