Esther lungu mama wa taifa zambia ashitakiwa kwa tuhuma za wizi

Kesi dhidi ya aliyekuwa Mama wa Taifa wa Zambia Esther Lungu, mke wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Edgar Lungu, imeanza mjini Lusaka.

Anashitakiwa kwa tuhuma za wizi wa magari matatu, wizi wa hatimiliki ya mali huko Lusaka na kupatikana na $400,000 zinazodaiwa kuwa mapato ya uhalifu, Anakabiliwa na kesi pamoja na maafisa wawili wa polisi.

Shahidi aliiambia mahakama Jumatatu kwamba Bi Lungu alichukua kwa nguvu gari lake na hati miliki ya nyumba yake pamoja na magari mawili ya binti yake.

Aliongeza kuwa maafisa wa polisi walioshtakiwa waliwalazimisha kutia sahihi hati za mali hizo kwa Bi Lungu.

Bi Lungu na washtakiwa wenzake walikanusha makosa walipokamatwa kwa madai ya makosa hayo mnamo Septemba.

Share: