Waziri mkuu wa uingereza keir starmer kufanya mkutano wa dharura

Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer anatazamiwa kufanya mkutano wa dharura baadaye - kufuatia wikendi ya machafuko yaliyoshuhudiwa katika maeneo tofauti nchini humo.

Polisi walikabiliana na matukio ya vurugu katika miji ya Rotherham, Middlesbrough na Bolton siku ya Jumapili - huku zaidi ya watu 150 wakisadikiwa kukamatwa.

Katika hotuba kwa taifa kupitia televisheni hapo jana, Keir Starmer alisema "watu katika nchi hii wana haki ya kuwa salama, na bado tunaona jumuiya za Kiislamu zikilengwa, katika mashambulizi dhidi ya misikiti".

Yote hayo yanafuatia shambulio la kisu huko Southport wiki iliyopita, ambalo lilisababisha watoto watatu (wenye umri wa miaka sita, saba na tisa) kuuawa.

Wengine watano walijeruhiwa, pamoja na watu wazima wawili.

Madai ya uwongo yalifuata kwamba mshukiwa - mwenye umri wa miaka 17 aliyezaliwa Cardiff kwa washirika wa Rwanda - alikuwa mkimbizi ambaye aliwasili Uingereza kwa boti mwaka 2023 na uvumi usio na msingi kuwa alikuwa Muislamu.

Mvulana huyo, Axel Muganwa Rudakubana, ameshtakiwa kwa makosa matatu ya mauaji, 10 ya kujaribu kuua na moja la kupatikana na kisu na anazuiliwa rumande ya vijana.

Share: