Waziri mkuu wa pakistan imran khan amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela

Aliyekuwa waziri mkuu wa Pakistan Imran Khan amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela katika kesi ambayo alishtakiwa kwa uvujaji wa siri za serikali.

Bw Khan, ambaye alitimuliwa na wapinzani wake kama Waziri Mkuu mnamo 2022, tayari anatumikia kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia ya ufisadi.

Ametaja mashtaka yote dhidi yake kuwa ya kisiasa.

Hukumu chini ya sheria ya siri inawadia wiki moja kabla ya uchaguzi mkuu ambapo amezuiwa kugombea.

Waziri wa zamani wa mambo ya nje Shah Mahmood Qureshi - makamu mwenyekiti wa chama cha Bw Khan cha Pakistan Tehreek-e-Insaf (PTI) - pia alihukumiwa kifungo cha miaka 10 jela na mahakama maalum.

Kinachojulikana kama kesi ya siri inahusu madai ya uvujaji wa barua za siri za kidiplomasia zilizotumwa na balozi wa Pakistan mjini Washington kwenda Islamabad wakati Bw Khan alipokuwa waziri mkuu.

Inahusiana na kuonekana kwake katika mkutano wa Machi 2022, mwezi mmoja kabla ya mchezaji huyo wa zamani wa kriketi kuondolewa mamlakani kwa kura ya kutokuwa na imani naye. Imran Khan alionekana jukwaani, akipunga karatasi ambayo anasema ilionyesha njama za kigeni dhidi yake.

Share: