Waziri mkuu wa israel netanyahu ametangaza mpango wa kupiga marufuku kituo cha habari al jazeera nchini humo

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametangaza mpango wa "kupiga marufuku mara moja" kituo cha habari maarufu kutoka nchini Qatar, Al Jazeera na kwamba ni chombo cha habari cha kigaidi.

Netanyahu ameahidi kuchukua hatua mara moja kutekeleza marufuku ya matangazo nchini Israeli ya kituo cha habari cha Al Jazeera.

"Kituo cha Al Jazeera hakitakuwa kinarusha matangazo kutoka Israeli, Nina nia ya kuchukua hatua mara moja kulingana na sheria mpya kusitisha shughuli za kituo," Waziri Mkuu wa Israeli alisema kwenye X.

Waziri wa Mawasiliano wa Israeli Shlomo Karhi alisema kuwa mashirika mengine ya matangazo ambayo nchi inayaona kuwa "yana uhasama" kwa Israeli katika kuripoti kuhusu mgogoro wa Gaza pia yatazuiwa kufanya kazi nchini.

Wanajeshi wa Israeli wameua takribani watu 32,845 huko Gaza tangu Oktoba 7, 2023.

Share: