Wanasiasa 16 wajitokeza kuwania urais wa urusi machi, 2024

Shirika la Habari la Urusi, RIA, limemnukuu kiongozi wa tume ya uchaguzi ya nchi hiyo Ella Pamfilova akitoa tangazo hilo hii leo, wiki moja kabla ya siku ya mwisho ya wagombea kujisajili ambayo ni Desemba 27.

Rais Putin tayari alitangaza mapema mwezi huu dhamira ya kuwania muhula wa tano katika uchaguzi uliopangwa kufanyika kwa muda wa siku tatu kuanzia Machi 15 mwaka 2024.

Kwa miaka kadhaa sasa utawala mjini Moscow umekuwa ukifanya ukandamizaji dhidi ya viongozi wa upinzani hususani nyakati za uchaguzi, mwenendo unaomsafishia njia kila wakati Rais Putin kupata ushindi wa kishindo.

Share: