WAASI WA HOUTHI WAVAMIA MAJENGO YA UN NCHINI YEMEN

Waasi wa Yemen wa Houthi wanaoungwa mkono na Iran walivamia ofisi za Umoja wa Mataifa katika mji mkuu wa Yemen Sanaa siku ya Jumapili na kuwaweka kizuizini takriban wafanyakazi 11 wa Umoja huo, shirika hilo lilisema.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alisema Wahouthi waliingia kwa nguvu katika majengo ya Mpango wa Chakula Duniani (WFP), wakachukua mali ya Umoja wa Mataifa na kujaribu kuingia katika ofisi nyingine za Umoja huo katika mji mkuu.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alisema Wahouthi waliingia kwa nguvu katika majengo ya Mpango wa Chakula Duniani (WFP), wakachukua mali ya Umoja wa Mataifa na kujaribu kuingia katika ofisi nyingine za Umoja huo katika mji mkuu.

Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa Yemen Hans Grundberg alisema katika taarifa tofauti kwamba wafanyakazi11 wanazuiliwa huko Sanaa na mji wa bandari wa Hodeidah.

Grundberg alisema kuzuiliwa kwao ni pamoja na wafanyikazi wengine 23 wa UN waliowekwa kizuizini hapo awali, wengine tangu 2021, na mmoja ambaye alikufa kizuizini mwaka huu.


Share: