Vitambulisho vya nida kuanza kugaiwa leo dar

Baada ya kusubiri kwa muda mrefu hatimaye wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wallojiandikisha kupata vitambulisho vya Taifa wanatarajia kuanza kuvipata kuanzia leo Desemba 12.

Matumaini hayo yamekuja kufuatia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kutoa taarifa kwa umma inayowataarifu wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kujiandaa kupokea vitambulisho vyao.

Taarifa hiyo ya Nida iliyotolewa na kitengo cha mawasiliano jana Jumatatu Desemba 11, 2023 imeeleza kuwa ugawaji wa vitambulisho kwa wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam utaanza leo na itadumu kwa siku 14.

Share: