Somalia inasema haitaongeza tena mamlaka ya ujumbe wa umoja wa mataifa nchini humo.

Waziri wa Mambo ya Nje ameliambia Baraza la Usalama kwamba serikali yake ina imani katika juhudi zake za kudumisha amani na ustawi kufuatia miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe na mashambulizi yanayohusiana na ugaidi.

Ujumbe huo sasa unatarajiwa kumaliza muda wake mwezi Oktoba kwa ombi la nchi hiyo.

Katika barua kwa baraza la usalama, Waziri wa Mashauri ya Kigeni Mohamed Fiqi anasema uamuzi huo umeafikiwa baada ya kuzingatia kwa kina vipaumbele vya serikali yake.

Bw.Fiqi anasema ujumbe huo umekuwa na mchango mkubwa kueleka upatikanaji wa amani, utulivu na maendeleo nchini.

Pia ameutaka ujumbe huo kuanza taratibu za kusitisha shughuli zake.

Serikali ya Rais Hassan Sheikh imekuwa katika harakati ya kuifanya Somalia kuwa taifa lenye utulivu na amani baada ya miaka mingi ya ukosefu wa utulivu.

Share: