Senegal: ousamne sonko na mwenzake bassirou diomaye faye wameachiwa huru kutoka gerezani

Kiongozi wa Upinzani, Ousamne Sonko na mwenzake Bassirou Diomaye Faye wameachiwa huru kutoka Gerezani kufuatia Sheria ya Msamaha iliyopitishwa na Bunge Machi 6, inayojaribu kupunguza ghasia baada ya mpango wa Rais wa kuahirisha Uchaguzi mpaka Desemba kukwama

Faye tayari ameteuliwa kuwa Mgombea Urais wa Upinzani katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Machi 24, 2024 baada ya Sonko kuzuiwa kuwania nafasi hiyo

Sonko aliyeshika nafasi ya 3 katika Uchaguzi wa Mwaka 2019 anachukuliwa kuwa tishio kubwa kwa Chama cha Rais Macky Sall, ambaye hagombei tena baada ya Maandamano ya kumpinga kwa Miezi kadhaa

Share: