Sababu za usalama zapelekea kucheleweshwa kwa kikao cha kinidhamu cha zuma

Chama tawala nchini Afrika Kusini, African National Congress (ANC), kimeahirisha kikao cha kinidhamu dhidi ya rais wa zamani Jacob Zuma kutokana na wasiwasi wa kiusalama.

ANC ilikuwa imemshtaki rais huyo wa zamani kwa kukiuka katiba ya chama kwa kukumbatia chama kipya cha Umkhonto we Sizwe (MK).

Chama cha MK, kinachoongozwa na Bw Zuma, kimepewa jina la tawi la zamani la kijeshi la ANC.

Alikuwa ameratibiwa kufika mbele ya kamati ya nidhamu ya chama siku ya Jumanne lakini hilo litafanyika baadaye baada ya uchaguzi.

Katibu Mkuu wa ANC, Fikile Mbalula alisema Jumapili kwamba ofisi yake imeshauriwa dhidi ya kufanya vikao vyovyote kwani vinaweza "kuvutia mikusanyiko mikubwa ambayo inaweza kusababisha vurugu au usumbufu... hasa karibu na siku ya uchaguzi".

Afrika Kusini inatazamiwa kufanya uchaguzi mkuu tarehe 29 Mei.

Hatua za kinidhamu zilipaswa kufanywa baada ya Bw Zuma kutangaza kuwa angepiga kura dhidi ya ANC katika uchaguzi huo, huku akiwa bado mwanachama.

Alikuwa ameshtakiwa kwa kukiuka katiba ya chama, na alisimamishwa Januari.

Hatua za kinidhamu zilipaswa kuchukuliwa baada ya Bw Zuma kutangaza kuwa angepiga kura dhidi ya ANC katika uchaguzi huo, huku akiwa bado mwanachama.

Alikuwa ameshtakiwa kwa kukiuka katiba ya chama.

Bw Zuma, ambaye alikuwa rais kutoka 2009 hadi 2018, bado ana nguvu kubwa ya kisiasa nchini Afrika Kusini.











Share: