Rais wa marekani joe biden amefanya mazungumzo na maafisa usalama wa marekani

Rais wa Marekani Joe Biden amekutana na timu yake ya masuala ya usalama wa taifa siku ya Jumatatu huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu uwezekano wa mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran dhidi ya Israel.

Bw Biden alisema alikuwa amefahamishwa kuhusu maandalizi ya kuunga mkono Israel iwapo itashambuliwa, huku Waziri wa Mambo ya Nje Antony Blinken akisema maafisa walikuwa wakifanya kazi "usiku na mchana" ili kuzuia kuongezeka.

Mvutano uliongezeka wiki iliyopita baada ya mauaji ya kiongozi wa kisiasa wa Hamas Ismail Haniyeh, ambapo Iran imeilaumu Israel na kuapa kulipiza kisasi "kikali".

Israel haijadai kuhusika na mauaji hayo.

Nchi nyingi, ikiwa ni pamoja na Marekani na Uingereza, pia wamewaambia raia wao kuondoka Lebanon, kukiwa na hofu kuwa Hezbollah inaweza kuchukua hatua yoyote kujibu mashambulizi.

Wakati wa mkutano wa Jumatatu, Bw Biden aliambiwa wakati na asili ya shambulio la Iran bado haijulikani, kulingana na tovuti ya habari ya Marekani ya Axios.

Siku moja kabla, Bw Blinken aliripotiwa kuwaambia viongozi wenzake wa G7 kwamba Iran na Hezbollah zinaweza kushambulia Israel ndani ya saa 24 hadi 48.

Share: