Rais mstaafu dkt. kikwete na afisa mtendaji mkuu wa gpe wakoshwa na utekelezaji mradi

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ushirikiano wa Elimu Duniani (GPE), Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa GPE, Bibi Laura Frigenti, leo wametembelea na kukagua shule za Msingi ya Maji Matitu iliyoko Mbagala na Mikongeni iliyoko Gongo la Mboto jijini Dar es salaam.

Katika ziara hiyo, iliyofanyika siku tatu kabla ya mkutano wa Bodi ya GPE utakaofanyika Zanzibar kuanzia mapema wiki ijayo, wamejionea shule ambazo Shirika hilo lImefadhili miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Madarasa, Vyoo na Mafunzo endelevu ya Walimu kazini na kueleza kuridhishwa na utekelezaji.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa GPE Bibi Frigenti ametoa wito kwa wadau wa maendeleo kuendelea kusaidia juhudi za kuendeleza sekta ya Elimu katika nchi zenye uhitaji, akisisitiza kwamba changamoto nyingi za kimaisha zinaweza kuepukika endapo wananchi watapatiwa elimu bora.

Bi. Frigenti ameeleza kuridhishwa na matumizi ya Fedha ambayo GPE imekuwa ikitoa kwa Tanzania na kuahidi kuendeleza uhusiano mzuri uliopo na uliodumu kwa miaka 10 sasa.

Share: