Nigeria: yaharibu tani 2.5 za meno ya tembo

Nigeria siku ya Jumanne iliharibu tani 2.5 za meno ya tembo yaliyokamatwa yenye thamani ya zaidi ya naira bilioni 9.9 (dola milioni 11.2) katika harakati za kulinda idadi yake ya tembo inayopungua dhidi ya walanguzi wa wanyamapori waliokithiri.

Katika miongo mitatu iliyopita, idadi ya tembo wa Nigeria imepungua kwa kiasi kikubwa kutoka makadirio ya 1,500 hadi chini ya 400 kutokana na ujangili wa pembe za ndovu, upotevu wa makazi na migogoro baina ya wanyama pori na binadamu, kulingana na wahifadhi.

Share: