Nigeria imeanzisha ushuru wa lazima kwa wafanyikazi kutoka nje

Nigeria imeanzisha ushuru wa lazima wa kila mwaka kwa mashirika yanayoajiri wafanyikazi kutoka nje, inayowahitaji kulipa $15,000 (£12,000) kwa watu wenye cheo cha mkurugenzi na $10,000 kwa vitengo vingine..

Hatua hiyo inakusudiwa kuhimiza makampuni ya kigeni kuajiri wafanyakazi zaidi wa Nigeria.

Wafanyikazi wa balozi za kidiplomasia na maafisa wa serikali hawatahitajika kulipa tozo hiyo.

Rais Bola Tinubu ameonya kuwa ushuru huo haufai kutumika kuwakatisha tamaa wawekezaji watarajiwa.

Alizungumza wakati akizindua kitabu cha Mwongozo cha Ushuru wa Ajira kwa Wageni (EEL) Jumanne, na kuongeza kuwa serikali inatarajia kuboresha mapato na ukuzaji.

Alisema kuwa lengo lake lilikuwa kusawazisha fursa za ajira kati ya Wanigeria na wahamiaji kutoka nje.

"Lengo ni kuziba mapengo ya mishahara kati ya wahamiaji kutoka nje na nguvu kazi ya Nigeria huku ikiongeza nafasi za ajira kwa Wanigeria waliohitimu katika makampuni ya kigeni nchini," alisema.

Share: