Namibia: rais hage geingob anatarajia kuanza matibabu ya saratani nchini marekani ikiwa ni siku chache tangu serikali ithibitishe

Rais Hage Geingob anatarajia kuanza Matibabu ya Saratani Nchini Marekani ikiwa ni Siku chache tangu Serikali ithibitishe kuwa Uchunguzi wa Kiafya umebaini ana Ugonjwa wa Saratani

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais, imesema shughuli zote za Urais zitakuwa chini ya Makamu wa Rais Nangolo Mumba hadi Februari 2, 2024

Serikali ya Namibia imekuwa ikiweka wazi hatua zote za hali ya Kiafya ya Rais Geingob ikiwemo ya kugundulika kuwa ana tatizo la Saratani ya Tezi Dume pamoja na kufanyiwa upasuaji wa Mishipa ya Damu kwenye Moyo

Share: