Mwanzilishi wa sarafu ya kidigitali sam bankman-fried ahukumiwa kifungo cha miaka 25 jela kwa utapeli

Sam Bankman-Fried, mwanzilishi mwenza wa shirika la kubadilishana fedha la crypto FTX, amehukumiwa kifungo cha miaka 25 jela kwa kuwatapeli wateja na wawekezaji wa kampuni yake ambayo sasa imefilisika.



Uamuzi huo unathibitisha kuanguka kwa bilionea huyo wa zamani, ambaye aliibuka kama bingwa wa hadhi ya juu wa sarafu ya crypto kabla ya kufilisika kwa kampuni yake mnamo 2022.
Alipatikana kuwa ameiba mabilioni ya wateja kabla ya kufilisika kwa kampuni hiyo.
Timu ya wanasheria ya Bankman-Fried itakata rufaa dhidi ya hukumu yake.
Ujumbe kutoka kwa wazazi wake ulioshirikishwa na BBC na mwakilishi wa Bankman-Fried ulisema: "Tumevunjika moyo na tutaendelea kumpigania mtoto wetu."
Awali, kijana huyo mwenye umri wa miaka 32 alisema mahakamani kwamba alijua "watu wengi" walihisi "kukatishwa tamaa".

"Samahani kwa hilo. Samahani kwa kile kilichotokea katika kila hatua," alisema, akizungumza kwa upole na uwazi kabla ya hukumu yake.

Kampuni ya FTX ilikuwa mojawapo ya ubadilishanaji mkubwa zaidi wa sarafu ya mtandaoni ya crypto ulimwenguni kabla ya kufilisika kwake, na kumgeuza Bankman-Fried kuwa mtu mashuhuri wa biashara na kuvutia mamilioni ya wateja ambao walitumia jukwaa la kampuni kununua na kufanya biashara ya cryptocurrency.

Uvumi wa matatizo ya kifedha ulisababisha watu kukimbia kutoa pesa zao mwaka wa 2022, na kusababisha kufilisika kwa kampuni hiyo pamoja na kufichua uhalifu wa Bankman-Fried.

Alipatikana na hatia na mahakama ya mjini New York mwaka jana kwa mashtaka yakiwemo ya ulaghai na kula njama ya kutakatisha fedha, baada ya kesi iliyoeleza jinsi alivyochukua zaidi ya $8bn (£6.3bn) kutoka kwa wateja, na kutumia pesa hizo kununua mali, kutoa michango ya kisiasa na uwekezaji mwingine.








Share: