Mpango wa paset kuiwezesha afrika kufikia malengo ya milenia

Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano ya Korea Kusini na Serikali za Afrika kupitia Mpango wa Afrika wa Sayansi, Uhadinsi na Teknolojia PASET umeandaa mkakati wa kuwawawezesha waafrika kukabiliana na changamoto mbalimbali zikiwemo za Magonjwa yasiombukiza na mlipuko, lengo ni kulifanya Bara la Afrika kuweza kutatua changamoto zake lenyewe.

Mpango huo umeanza mwaka 2018 na utadumu kwa zaidi ya miaka 10 unalenga kufadhili masomo ngazi ya uzamivu (PHD) kwa wananfunzi elfu kumi ambapo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo ( SUA) ni moja kati ya vyuo vikuu vya mwanzo kushiriki katika mpango huo kati ya vyuo vikuu 15 barani Afrika.

Mratibu wa Mpango wa Afrika wa Sayansi, Uhadinsi na Teknolojia PASET kutoka SUA Prof. Gerald Misinzo amesema mpaka sasa SUA imepokea wananfunzi 43 kutoka Nchi mbalimbali za Bara la Afrika ikiwemo Tanzania, Kenya, Rwanda, Malawi, Msumbiji, Chadi, Benin, Sudan ya Kusini na Nigeria.

Amesema Wanafunzi hao, watasoma Teknolojia, Sayansi pamoja na Uhadinsi, lengo ni kutatua changamoto za milenia ili kufikia malengo ya Afrika kufikia 2023 ya kila Mwafrika kuwa na Afya bora, kupunguza umasikini na kuwa na uhakika wa chakula.

Share: