meli za kivita za urusi zimeondoka katika bandari ya havana baada ya ziara ya siku tano

Meli za meli za kivita za Urusi zimeondoka katika bandari ya Havana baada ya ziara ya siku tano nchini Cuba, kufuatia mazoezi ya kijeshi yaliyopangwa.

Meli hizo, ambazo ni pamoja na manowari inayotumia nguvu za nyuklia, zilikuwa zimetia nanga katika Ghuba ya Havana - takriban maili 90 (145km) kutoka jimbo la Florida nchini Marekani.


Marekani ilisema kuwa haioni hilo kama tisho, lakini ikaongeza kuwa inafuatilia meli hizo kwa karibu.

Kufuatia meli hiyo kuwasili, Marekani ilitia nanga manowari yake, USS Helena, katika Kambi yake ya Wanamaji ya Guantanamo huko Cuba siku ya Alhamisi.

Wenyeji walipeperusha bendera za Urusi huku meli za Urusi zikiondoka Jumatatu.

Wizara ya mambo ya nje ya Cuba ilisema hakuna meli hiyo iliyo na silaha za nyuklia, na ziara hiyo haina tishio kwa eneo hilo.

Lakini wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema meli ya Admiral Gorshkov na manowari ya Kazan zote ni za kubeba silaha za hali ya juu, ikiwa ni pamoja na makombora ya hypersonic Zircon. Hapo awali walifanya mazoezi ya kombora katika Atlantiki.

Urusi ilituma meli za kivita nchini Cuba hapo awali na mataifa hayo mawili ni washirika wa muda mrefu - lakini muda wa mazoezi haya ni hanadhihirika wazi.

Share: