Mahakama ya serikali kuu ya pakistan imebatilisha hukumu ya nawaz sharif

Chama chake cha Pakistan Muslim League-N (PML-N), kinasema mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 73 anapanga kuwania tena nafasi ya Waziri Mkuu kwa mara ya nne.

Mahakama moja ya serikali kuu ya Pakistan imebatilisha hukumu ya Waziri Mkuu wa zamani, Nawaz Sharif katika kesi ya mwisho ya ufisadi, ambayo inamsogeza karibu na kuwania uchaguzi mkuu mwezi Februari.

Sharif amehudumu kama Waziri Mkuu wa Pakistan kwa mihula mitatu isiyo ya kisheria. Sharif alirejea Pakistan mwezi Oktoba baada ya kuishi uhamishoni kwa miaka minne mjini London, akiepuka kutumikia kifungo cha miaka 10 jela kwa tuhuma za rushwa.

Chama chake cha Pakistan Muslim League-N (PML-N), kinasema mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 73 anapanga kuwania tena nafasi ya Waziri Mkuu kwa mara ya nne. Mahakama kuu katika mji mkuu Islamabad, ilitangaza uamuzi wake siku ya Jumanne kujibu rufaa ya Sharif, ambayo aliiwasilisha dhidi ya hukumu yake muda mfupi baada ya kurejea Pakistan.

Share: