Maelfu waandamana serbia kupinga udanganyifu kwenye uchaguzi

Kwa takriban Wiki 2 sasa, Maelfu ya Wananchi wamekuwa wakiandamana katika Mji Mkuu, Belgrade, wakimshutumu Rais Aleksandar Vucic kufanya Udanganyifu wakati wa Uchaguzi wa Bunge na Serikali za Mitaa wa Desemba 17, 2023

Chama Tawala cha Serbian Progressive Party kilitangazwa kuwa Mshindi lakini Muungano wa Upinzani wa Serbia Against Violence, unadai kuwepo wizi wa kura na umeomba Tume ya kuchunguza kasoro hizo na ikiwezekana Uchaguzi urudiwe. 

Wakati Chaguzi zikiendelea katika Mataifa mbalimbali, Watanzania nao wanajiandaa kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Mwaka 2024 pamoja na Uchaguzi Mkuu wa 2025

Share: