
Irom Sharmila alianza mgomo wake wa kususia kula mnamo mwaka 2000 kupinga sheria yenye utata katika jimbo la kaskazini-mashariki la Manipur, ambayo iliipa nguvu zaidi jeshi la India.
Sheria hiyo inaruhusu wanajeshi wa India ambao wamepelekwa katika maeneo ambayo serikali inayachukulia kuwa "yenye vurugu" kukamata watu bila vibali na hata kupiga risasi kukusudia kuua katika hali fulani.
Mnamo mwezi Novemba 10, 2000, raia 10 waliokuwa wamesimama kwenye kituo cha mabasi katika Jimbo la Sharmila la Manipur walidaiwa kupigwa risasi na kuuawa na wanajeshi wa India ambao walidai walikuwa wakiwarushia risasi.
Tukio hilo, lililopewa jina la "mauaji ya Malom" na raia waliokuwa na hasira, na kuwa chanzo cha Sharmila kuanza mgomo wa kutokula. Aliapa kuendeleza mgomo huo hadi sheria hiyo itakapofutwa.
Bi Sharmila alipoanza tu mgomo huo, alikamatwa na kuwa hospitalini kwa miaka 16, akizungukwa na walinzi wenye silaha na timu ya madaktari na wauguzi ambao walimlazimisha kula virutubishi vya kioevu na dawa kwa njia ya bomba, wakati mwingine hadi mara tatu kwa siku.
Wakati huo wote, Sharmila alipata uungwaji mkono mkubwa ulimwenguni na hata alishinda tuzo bora kutoka kwa Tume ya Kutetea Haki za Binadamu ya Asia.
Mnamo tarehe 26 Julai 2016, Irom Sharmila, ambaye alikuwa kwenye mgomo wa kula tangu 2000, alitangaza kwamba atamaliza mgomo huo mnamo 9 Agosti 2017.
Na pia, alitangaza kuwa atagombea uchaguzi ujao wa serikali huko Manipur. Kusudi la kujitosa siasani haraka ilikiwa kupigania kuondolewa kwa sheria hiyo tata. Sharmila alisema "nitajiunga na siasa na jitihada zangu za kupinga sheri hili zitaendelea."