Ecowas 'bado haijapokea' notisi ya kujiondoa ya burkina faso, mali na niger

Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) imesema bado haijapokea notisi rasmi kutoka kwa Mali, Burkina Faso na Niger kutangaza kujiondoa kwenye umoja huo wa kikanda.

Nchi hizo tatu mapema Jumapili zilisema katika taarifa yake kwamba zinaondoka ECOWAS, na kusema kuwa shirika la kikanda limeshindwa kuwasaidia kutatua changamoto za ukosefu wa usalama, miongoni mwa masuala mengine.

"Tume ya ECOWAS bado haijapokea arifa yoyote rasmi ya moja kwa moja kutoka kwa nchi tatu wanachama kuhusu nia yao ya kujiondoa kutoka kwa jumuiya," ECOWAS ilisema katika taarifa iliyotumwa kwenye mtandao wa kijamii wa X.

Shirika la kikanda hata hivyo lilisema "lilikamatwa na maendeleo."ECOWAS iliongeza kuwa imekuwa "ikifanya kazi kwa bidii na nchi hizi kwa ajili ya kurejesha utaratibu wa kikatiba."

"Burkina Faso, Niger, na Mali zinasalia kuwa wanachama muhimu wa jumuiya na mamlaka inasalia na nia ya kutafuta suluhu la mkwamo wa kisiasa kwa njia ya mazungumzo."

ECOWAS ilisema itatoa matamko zaidi "kadiri hali inavyoendelea."

Katika taarifa ya pamoja siku ya Jumapili, Kapteni Ibrahim Traore wa Burkina Faso, Kanali Assimi Goita wa Mali, na Jenerali Abdourahamane Tchiani wa Niger walisema ni "uamuzi wao huru" kuondoka ECOWAS, na kuongeza kuwa kuondoka kwao "bila kuchelewa."

Nchi hizo ambazo ziko chini ya utawala wa kijeshi kufuatia mapinduzi tofauti, zimeishutumu ECOWAS kwa kuzilenga isivyo haki, hasa kuhusiana na hali ya kisiasa na kiusalama katika mataifa hayo matatu.

Share: