Drc congo: 15 jela baada ya kupatwa na hatia ya kufadhili ugaidi

Mahakama ya kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewahukumu watu 15 jela baada ya kuwapata na hatia ya kufadhili ugaidi kupitia biashara haramu ya dhahabu.

Mahakama hiyo mnamo Alhamisi iliwafunga washukiwa 10 kwa vifungo vya kati ya miaka mitano na minane na kuwapa wengine watano kifungo cha miaka 10.

Mahakama pia iliwaachia huru washtakiwa tisa.

Washtakiwa walisimama wakituhumiwa kuwezesha uhamishaji wa pesa zilizopatikana kutokana na uuzaji haramu wa dhahabu na vito vya thamani kwenda kwa vikundi vya wapiganaji.

Msemaji wa timu ya wanasheria wa washtakiwa alikanusha mashtaka na kuliambia shirika la habari la AFP kwamba watakata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Share: