Biden na xi wakubaliana kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano

Marais hao walikubaliana katika mkutano wao wa kwanza wa kilele kuandaliwa katika mwaka mmoja.

Biden na Xi walisalimiana kwa mikono kabla ya mazungumzo yao ya saa nne yaliyojikita katika kuzuia mivutano inayoongezeka kati ya madola hayo mawili makubwa duniani kugeuka kuwa mzozo mkubwa.

Pia walikubaliana kuwa China itadhibiti uzalishaji wa dawa za kulevya za opioid ambazo zimekuwa janga nchini Marekani. Rais Xi amesema China iko tayari kushirikiana na Marekani

Hata hivyo Xi na Biden waliendelea kutofautiana kuhusu suala la Taiwan, huku rais wa China akimtaka mwenzake wa Marekani kukoma kukipa kisiwa hicho silaha za kivita na kwamba suala la kuungana tena halizuiliki.

Hata hivyo, Biden baada ya mkutano huo aliwaambia waandishi wa habari kuwa bado anamzingatia Xi kuwa dikteta. Kauli hiyo imelaaniwa vikali na China.

Share: