Benki ya dunia kuchunguza mradi wa upanuzi hifadhi ya ruaha

Hatua hiyo inatokana na Ripoti ya Taasisi ya Oakland iliyoandikwa kwa niaba ya Wanakijiji wa Wilaya ya Mbarali wanaodai kuathiriwa na zoezi la kuhamishwa kupisha upanuzi wa Hifadhi ya Kitaifa ya Ruaha (RUNAPA) chini ya Mradi wa REGROW ambao unafadhiliwa na Benki ya Dunia

Jopo la Ukaguzi (IP) ambalo limepokea Ripoti hiyo limependekeza Uchunguzi wa mapitio ya Benki ikiwemo ya Wakala Mkuu wa Utekelezaji wa Mradi huo, Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), pia ichunguze ukiukwaji wa sera zinazotumika na Benki ya Dunia

Dola Milioni 92 (Tsh. Bilioni 229) kati ya Dola Milioni 150 (Tsh. Bilioni 374) za Mradi zimeshatolewa. 

Share: