Diamond na zuchu ni masuper star wa muziki nchini Tanzania,Africa na ulimwenguni kwa ujumla ,wameacha mashabiki na wadau wa muziki kwenye mataa baada ya gumzo liliopo mtandaoni kuhusu maudhui ya picha ,video na zile captions zinazo husisha uwepo wa ndoa ya mastar hao,ambapo mwanaharaki mwiba ,mdakuzi wa taarifa Mange Kimambi amedai kuwa...

Ndoa ya Diamond na Zuchu ni Ndoa ya mkeka amabayo ilishafungwa miezi iliopita tena kimya kimya ,na mpaka sasa Ndoa hii haina maisha akiwa anadai kuwa talaka tatu zimemuhusu Zuhura maarufu kwa jina la zuchu.

Kwenye kurasa za mitandao yao kijamii za wasanii hao wote wawili zimechapishwa video na picha zinazoonyesha kuwa Diamond na Zuchu kuwa ni mke na mume huku sheikh akionekana kwenye picha akifungisha Ndoa hio, Haijaishia hapo sheikh ametoa taarifa kuwa ndoa hio imefungwa takribani miezi mnne ilipiya kabla ya maudhui hayo yahusuyo ndoa kuzagaa mitandaoni mwishoni mwa mwezi wa Mei mwaka huu 2025.

Tazama video yenye taarifa zaidi kisha tuambie maoni yako kupitia mitandao yetu ya kijamii ,(facebook,instagram) @stbongo, kulingana na viashiria na tarifa zilizopo zinazo husu wuhusika wa karibu wa tukio hili kwa pande zote mbili za masuper star hao.

Share: