
Lil Wayne ametangaza rasmi ujio wa albamu yake ijayo “Tha Carter VI,” ambayo itatolewa mnamo Juni 6.
Rapa huyo alizua gumzo mapema jana Alhamis baada ya kudokeza kuhusu mradi huo mpya mwishoni mwa tangazo la Super Bowl kwa Cetaphil.
Ingawa haikueleweka wazi kama hilo lilimaanisha kuwa albamu hiyo itatolewa rasmi majira ya kiangazi, lebo yake Republic Records na Young Money baadaye zilithibitisha kuwa Wayne anajiandaa kuachia toleo jipya la mfululizo wake mashuhuri wa “Carter” katika miezi michache ijayo.
Kuonekana kwa Wayne kwenye tangazo hilo la Super Bowl kulionyesha hisia zake za kutoridhika kwa kutopata nafasi ya kutumbuiza katika Halftime Show ya mwaka huu, ambayo badala yake itamshirikisha Kendrick Lamar.
Mitandao ya kijamii iliibua maoni haraka kwamba Wayne alipaswa kupewa nafasi hiyo katika jiji lake la asili, New Orleans. Katika tangazo hilo, Wayne anatania kuhusu hali hiyo kwa kutumia kauli mbiu inayosema “sote tuna hisia kidogo.”
Imepita miaka saba tangu Wayne alipoachia “Tha Carter V,” toleo la tano katika mfululizo huo ulioanza mwaka 2004.
“TC5” ilikuwa mafanikio makubwa kwa Wayne, ikishika nafasi ya kwanza kwenye chati za Billboard 200 na kuzaa vibao kama “Uproar” na “Don’t Cry.” Wayne alidokeza kuhusu toleo la sita alipotoa “Tha Fix Before Tha VI” mnamo Septemba 2023, mixtape iliyowashirikisha Jon Batiste na Fousheé.