HAMISA MOBETTO ANAKULA SAHANI MOJA NA MKE WA RONALDO NA MESSI

Mwanamitindo kutoka Tanzania, @hamisamobetto ametajwa kwenye orodha ya wanawake 10 duniani wenye wafuasi wengi zaidi kwenye Instagram, ambao ni wake au wapenzi wa wachezaji wa soka maarufu duniani (wanaojulikana kama WAGs – Wives and Girlfriends of footballers).

Katika ripoti mpya iliyotolewa na jarida la GMSSTATS_HP, Hamisa ametajwa kushika nafasi ya nane duniani, akiwa na zaidi ya wafuasi milioni 12.2 kwenye mtandao wa Instagram. Anatajwa kama Mke wa nyota wa Waydad na mchezaji wa kimataifa wa Burkina Faso, Stephane Aziz Ki.


Orodha hiyo inaongozwa na Georgina Rodríguez, Mpenzi wa Cristiano Ronaldo, ambaye ameendelea kushika nafasi ya kwanza akiwa na zaidi ya wafuasi milioni 67, akifuatiwa na Antonela Roccuzzo, mke wa Lionel Messi, mwenye wafuasi milioni 40. Nyota wengine katika orodha hiyo ni pamoja na Becky G, Victoria Beckham, Bruna Biancardi(mpenzi wa Neymar), na wengine wengi kutoka sehemu mbalimbali za dunia.


Hii ndio orodha kamili:

1. Georgina Rodríguez – 67M

2. Antonela Roccuzzo – 40M

3. Becky G – 37M

4. Victoria Beckham – 32.9M

5. Tini Stoessel – 21.5M

6. Perrie Edwards – 18.9M

7.Bruna Biancardi – 13.8M

8. Hamisa Mobetto – 12.2M

9. Pilar Rubio – 11M

10. Leigh-Anne Pinnock – 9.8M



Share: