Daftari la mistari ya lil wayne kuuzwa bilioni 14

Daftari la zamani la Lil Wayne la miaka ya 90 ambalo alikuwa analitumia kuandikia mashairi ya ngoma zake limewekwa sokoni na sasa linauzwa kwa $5 milioni (Bilioni 13 TSH)

Kulingana na TMZ, tovuti ya kumbukumbu ya mtandaoni ya Moments In Time ilipigana kwa miaka mitano kuthibitisha kwamba walikuwa na haki ya kisheria ya kuuza daftari hilo, ambalo lilianzia siku za mwanzo za Weezy kama mwanachama wa Hot Boys katika miaka ya 90.

Jukwaa hilo hapo awali liliorodhesha daftari hilo mnamo 2019, kwa niaba ya mtu ambaye alidai kuwa alipata maandishi ya Lil Wayne yaliyoandikwa kwa mkono kwenye gari ambalo lilikuwa la Cash Money Records. Mara tu bidhaa hiyo ilipoorodheshwa, hata hivyo Weezy aliitaka kampuni hiyo kusitisha mnada huo , akitaka daftari hilo lirudishwe kwake.

Februari, Jaji Kern A. Reese Orleans huko Louisiana aliamua kwamba Moments In Time walikuwa na haki zote za kuuza daftari, kulingana na hati ya kisheria iliyochapishwa kwenye ukurasa wa mauzo, Bei ya sasa ya daftari ni mara 20 zaidi ya bei yake ya awali ya $250,000.

Share: