Nape nnauye: gharama za data (intaneti) ndani ya kifurushi zimeshuka kwa kiasi kidogo na kufikia wastani wa tsh. 2.17 kwa megabyte

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, amesema katika robo ya Mwaka inayoishia Machi 2024, gharama za Data (Intaneti) ndani ya kifurushi zimeshuka kwa kiasi kidogo na kufikia wastani wa Tsh. 2.17 kwa Megabyte ikilinganishwa na Tsh. 2.25 ya Juni, 2023

Akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya hiyo Bungeni, Nape amesema wastani wa Bei ya kupiga Simu ndani ya Mtandao mmoja kwa Dakika 1 imeshuka kutoka Tsh. 29 Juni 2023 hadi Tsh. 26 huku Bei ya kupiga Simu nje ya Mtandao kwa Aprili 2024 ikifikia Tsh. 28 kutoka Tsh. 31 ya Juni 2023

Share: