Mfanyabiashara bilionea wa marekani larry connor anapanga kusafiri chini ya maji kwa kutumia manuwari hadi ilipo meli ya titanic

Mfanyabiashara bilionea wa mali isiyohamishika wa Marekani na tajiri na msafiri wa Ohio Larry Connor, Patrick Lahey, mwanzilishi mwenza wa Manowari ya Triton, wanasema wanataka kusafiri chini ya bahari hadi kina cha karibu 3,800m (12,467ft) ili kuona ajali ya meli ya Titanic katika Bahari ya Atlantiki Kaskazini.


Sekta ya kibinafsi ya safari ya chini ya maji ilitikisika baada ya watu watano kupoteza maisha wakati meli iliyojengwa na Ocean Gate ilipokwama ilipokuwa ikielekea Titanic mwaka jana.

Msemaji wa kampuni ya Bw.Connor alisema Jumanne kwamba safari iliyopendekezwa itafanyika mara tu chombo kitakapoidhinishwa kikamilifu na shirika la wanamaji.


Hakuna muda uliopangwa wa safari. Wawili hao wanapanga kutumia manuwari ndogo inayoitwa Triton 4000/2 Abyssal Explorer - "4000" kinachoweza kwenda kina cha umbali ambao chombo kinaweza kwenda kwa usalama.

Manowari ya Titan iliyojengwa na Ocean Gate ilitengenezwa kwa nyuzinyuzi za kaboni na iliidhinishwa tu hadi mita 1,300, kina fupi sana cha sakafu ya bahari ambapo mabaki ya meli ya Titanic yapo.

Share: