Mamilioni ya watu wanatumia mbinu za kiufundi kuitumia whatsapp kwa siri katika nchi ambazo imepigwa marufuku

Mamilioni" ya watu wanatumia mbinu za kiufundi kufikia WhatsApp kwa siri katika nchi ambazo imepigwa marufuku, bosi wa jmtandao huo amesema.

"Utashangaa ni watu wangapi wamegundua," Will Cathcart .

Kama programu nyingi za Magharibi, WhatsApp imepigwa marufuku nchini Iran, Korea Kaskazini na Syria.

Na mwezi uliopita, China ilijiunga na orodha ya wale wanaopiga marufuku watumiaji kufikia mtandao huo ulio salama.

Nchi nyingine, ikiwa ni pamoja na Qatar, Misri, Jordan na Umoja wa Falme za Kiarabu, huweka vikwazo kwa vipengele kama vile simu za sauti.Lakini WhatsApp inaweza kuona ni wapi watumiaji wake wapo, kutokana na nambari zao za simu zilizosajiliwa."

Tuna ripoti nyingi za watu wanaotumia WhatsApp na tunachoweza kufanya ni kuangalia baadhi ya nchi ambazo tunazuiwa na bado tunaona makumi ya mamilioni ya watu wakitumia WhatsApp," Bw Cathcart.

Acha kitu'China iliiamuru Apple kuwazuia watumiaji wa iPhone wa China kupakua WhatsApp kutoka kwa AppStore mwezi Aprili, hatua ambayo Bw Cathcart anaiita "ya kushangaza" - ingawa nchi hiyo haikuwa soko kuu la programu hiyo."

Hilo ni chaguo Apple imefanya," alisema."Hakuna njia mbadala."

Namaanisha, hiyo ni hali ambayo wamejiweka katika nafasi ya kuweza kukomesha kitu"Watumiaji wa Android, hata hivyo, bado wanaweza kupakua WhatsApp bila kupitia maduka rasmi.

Lakini kwingineko Bw Cathcart alisema kuongezeka kwa mitandao ya kibinafsi (VPNs) na huduma ya wakala ya WhatsApp, iliyozinduliwa Juni mwaka jana, kumesaidia kufanya WhatsApp ipatikane.

Share: