Wapiga kura wa chama cha democratic wanazidi kuwa na wasiwasi kuhusu umri wa joe biden

Kura mpya ya maoni inapendekeza kwamba baadhi ya wapiga kura wa chama cha Democratic wanazidi kuwa na wasiwasi kuhusu iwapo Joe Biden yuko sawa kiakili kuhudumu kama rais baada ya kuyumba kwenye mjadala siku ya Alhamisi.

Kura ya maoni ya CBS News/YouGov iliyotolewa Jumapili ilionyesha kuwa 72% ya wapiga kura waliojiandikisha wanaamini kuwa Biden hana uwezo wa afya ya kiakili ya kuhudumu kama rais - ongezeko kubwa kutoka 65% kwa waliokuwa na maoni kama hayo katika kura ya maoni ya awali.

Asilimia 49 ya wapiga kura walikuwa na maoni kama hayo kwa Rais wa zamani Donald Trump.

Hasa jambo la kutia hofu kwa kampeni ya Biden, 45% ya Wanademokrasia waliojiandikisha ambao walijibu kura hiyo walisema wanaamini kuwa rais anapaswa kujiondoa na mgombea mwingine kuchukua nafasi yake.

Bw Biden ana miaka 81 na Trump ana miaka 78. Sauti ya kishindo ya Bw Biden na majibu ya kutatanisha, hata hivyo, yalizua wasiwasi miongoni mwa baadhi ya Wanademokrasia kuhusu kugombea kwake na kuwaacha wengine wakitaka Bw Biden ajiondoe kwenye ugombeaji.

Familia ya rais ilimtia moyo kusalia katika kinyang'anyiro hicho wakati wa ziara iliyopangwa kwa muda mrefu huko Camp David siku ya Jumapili, chanzo chenye kufahamu mazungumzo hayo kilithibitishwa na CBS News, mshirika wa BBC wa Marekani.

Bado, mbunge wa Maryland, Jamie Raskin ambaye pia ni mshirika wa Democrat na White House, alielezea mahojiano yake kama "wakati mgumu".

Raskin alisema kuna "mazungumzo ya ukweli na mazito yanayofanyika katika kila ngazi ya chama chetu", ingawa alisisitiza kuwa uamuzi wa mwisho unasalia kuwa wa Bw Biden.

"Licha ya uamuzi wowote utakaochukuliwa na Biden, chama chetu kitakuwa na umoja na pia kinamhitaji katikati mwa mijadala yetu katika kampeni," aliongeza.

Share: