Wanaotaka kuandamana tutawalinda-rais samia

Tunaendelea kuimarisha uhuru wa kujieleza na kuhamasisha siasa za kistaarabu na zinazolenga kuleta maendeleo ya watu.

"Tunasisitiza kustahamiliana na kuzingatia sheria ili siasa zetu zisiwe chanzo cha mitafaruku au machafuko.

Vyama vya siasa vinaendelea kufanya shughuli zao kwa uhuru kabisa, wanaotaka kuandamana tunawaambia ingieni barabarani tutawalinda.

Wanakwenda weeh! mpaka wakichoka wanakokwenda, wanafika wanafanya yao... haya tawanyikeni, wanatawanyika"

Mtu anatamani kusema, tunamwambia kiwanja hiki hapa, jukwaa hili hapa, akimaliza! haya baba shuka nenda zako,anashuka anaenda zake"

Share: