Wagombea urais kongo watoa ahadi tele kuelekea uchaguzi mkuu

Wagombea urais nchini Kongo wametoa ahadi chungunzima kuelekea uchaguzi wa kesho Jumatano baada ya muda wa kufanya kampeni kukamilika rasmi jana katika hilo la Afrika ya Kati lenye idadi ya watu wapatao milioni 100.

Ikiwa imesalia siku moja tu kwa uchaguzi huo kufanyika, tayari wagombea kadhaa wa urais wamejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho na kuwaacha wagombea 18 akiwemo rais wa sasa Felix Tshisekedi wakiwania nafasi hiyo ya juu.

Raia milioni 44 wa Kongo wamejiandikisha kama wapiga kura katika uchaguzi wa kesho wa urais, bunge na udiwani.

Mbali na kunadi sera zao, wagombea hao walichukua muda mwingi kutupiana lawama na hata kauli nzito. Lakini miongoni mwa masuala yaliopewa kipau mbele ni suala la usalama. 

Wagombea wote wa urais wameahidi kumaliza vita na machafuko ya muda mrefu eneo la mashariki mwa Kongo.

Share: