
Zifahamu sifa za kuweza kugombea kiti cha Raisi wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania kwa mujibu wa sheria
Ikiwa huu ni mwaka 2025 ,nchini kwetu Tanzania ni mwaka wa uchaguzi wa vingozi kwanzia serekali za mtaa mpaka uongozi wa serekali kuu ,madiwani, wabunge na Raisi wa nchi. Tuchukue nafasi hii kufahamu sifa za kisheria za kuweza kugombea nafasi kiti ya Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Kwa mujibu wa kifungu cha 30 cha sheria ya taifa ya uchaguzi,sura ya 343 sifa za mgombea kiti cha Raisi kama ifwatavyo,
1. Awe ni raia wa kuzaliwa wa jamhuri ya mungano wa Tanzania.
2. Awe ametimiza umri wa miaka arobaini (40)
3. Awe mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa nchini.
4. Awe anazo sifa za kumwezesha kuwa mbunge au mjumbe wa baraza la wawakilishi na asiwe ametiwa hatiani na mahakama yoyote kwa kosa la kukwepa kulipa kodo yoyote ya serekali katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya uchaguzi.
Chanzo cha tarifa Tume huru ya Taifa ya uchaguzi
Asante sana kwa kufwatilia tovuti yetu www.stbongo.co.tz ,kaa tayari kupokea taarifa, matukio na mengine mengi tutakufikishia kidigital.