Rais mteule wa senegal bassirou diomaye faye alifungwa kwa takriban mwaka mmoja na kuachiliwa kufuatia msamaha wa rais.

Mgombea wa upinzani Bassirou Diomaye Faye aliibuka mshindi wa uchaguzi wa Jumapili kwa 54.28% ya kura zote, huku mpinzani wake mkuu, Waziri Mkuu wa zamani Amadou Ba wa muungano tawala, akipata 35.79% ya kura zote.

Idadi ya wapiga waliojitokeza kwa kura hiyo ilikuwa asilimia 61.

Rais Macky Sall alikuwa amejaribu kuchelewesha upigaji kura uliokuwa umepangwa kufanyika hapo awali Februari, jambo ambalo lilizua maandamano ya ghasia na kusababisha vifo vya watu watatu.


Baraza la uchaguzi nchini Senegal limemthibitisha mgombea wa upinzani Bassirou Diomaye Faye kuwa mshindi wa uchaguzi wa Jumapili.

Wapinzani wake wa kisiasa walikuwa wameanza kukubali kushindwa ndani ya saa chache baada ya zoezi la upigaji kura kufungwa.

Bw Faye aliibuka kutoka kwa mgombeaji maarufu wa upinzani Ousmane Sonko, ambaye aliondolewa kwa sababu ya hatia kumharibia mtu jina iliyositishwa.

Rais mteule alifungwa kwa takriban mwaka mmoja na kuachiliwa kufuatia msamaha wa rais.

Alikuwa na siku tisa tu za kufanya kampeni na sasa ni Rais mteule wa Senegal na ndiye mwenye umri mdogo zaidi kuchaguliwa kidemokrasia barani Afrika.

Ameahidi kupambana na ufisadi na kukabiliana na ukosefu wa ajira, pamoja na gharama kubwa ya maisha.

Share: